FLASH


Friday, April 5, 2013

UMOJA NI USHINDI KILA RAHELI NAPE

 KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI TAIFA NAPE NAUYE ATINGA MKOANI KILIMANJARO LEO KUUNGURUMA MOSHI KESHO 


 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akilakiwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Iddi Mohammed baada ya kuwasilili jioni hii kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo mjini Moshi. Kesho Nape anatarajiwa kufungua semina ya Halmashauri Kuu ya Mkoa huo ya CCM na baadaye kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Moshi.
 Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Steven Kazidi (wapili kushoto) akimtambulisha Mwenyekiti wa UVCCM mkoa huo, Frederick Mushi kwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Moshi Mjini Elizabeth Minde.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akivishwa skafu na Kijana wa CCM baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanajro mjini Moshi jioni hii.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kucharaza ngoma, iliyokuwa inapigwa na kundi la sanaa la CCM, baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro jini Moshi jioni hii.
 Katika ziara hiyo Nape ameambatana na Vijana waliojiengua hivi karibu kutoka Chadema, Mtela Mwampanga na aliyekuwa Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema, Juliana Shonza. Pichani, Mwampamba na Shonza wakisalimiana na vijana wenzao ambao pia wamehamia CCm hivi karibuni kutoka Chadema mkoani Kilimanjaro, David Waryoba (kushoto) na Yona Makwaya (wapili kushoto)
Vijana wakimsubiri Nape kwa shauku alipowasili Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi jioni hii.
Nape akitia saini kwenye kitabu cha wageni, katika Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro mjini Moshi jioni hii. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Iddi Mohammed.(Picha zote na Bashir Nkoromo)

PAMOJA NAKUAMUA KUTAFUTA UFUMBUZI CCM TUWE MAKINI KWENYE VYUO NA MATAMKO

CCM yaunda kamati kushughulikia mgogoro

                                     Naibu Katibu Mkuu Bara, Mwigulu Nchemba. 
0
Arusha. Chama Cha Mapinduzi (CCM) hatimaye kimeingilia kati mgogoro wa ardhi Loliondo, baada ya kuunda kamati maalumu kuchunguza mgogoro huo, itakayoongozwa na Naibu Katibu Mkuu Bara, Mwigulu Nchemba.

Wakati chama hicho kikichukua hatua hiyo, wanafunzi kutoka Wilaya ya Ngorongoro wanaosoma vyuo mbalimbali mkoani Arusha, wametangaza nia ya kuacha masomo warejee vijijini kutetea ardhi ya wazee wao.

Akizungumza mjini hapa juzi, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ngorongoro, Abraham Sakay alisema kutokana na mgogoro huo, waliamua kwenda kuonana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Sakay alisema CCM Ngorongoro, inaungana na wanachama kuipinga Serikali, kutwaa ardhi ya vijiji kilomita za mraba 1,500, lakini imeona siyo busara sasa viongozi wote wa kuchaguliwa ambao ni wa CCM kujiuzulu.

Viongozi wote wa kuchaguliwa katika wilaya hiyo, ambao wanatishia kujiuzulu wanatoka CCM.Sakay alisema viongozi wa kitaifa wa CCM, wanatarajiwa kufika wilayani humo mapema iwezekanavyo kuzungumza na viongozi wa wilaya na wanachama wa CCM.

Hata hivyo, wakati CCM ikiingilia kati mgogoro huo, juzi zaidi ya wanachama 200 wa CCM, walitupa kadi baada ya mkutano uliofanyika jirani na Uwanja wa Ndege Loliondo.
Akizungumza juzi, Mwenyekiti wa wanafunzi hao, Albert Selembo alisema vijana wanaotoka wilayani Ngorongoro wamesikitishwa na uamuzi wa Serikali.

Naye Katibu wa Umoja huo, Flavian Massango anayesoma Chuo Kikuu cha Makumira Arusha, alisema iwapo Serikali ya CCM ina mpango wa kutumia uhifadhi kwa kulaghai ardhi, hautafanikiwa.

Alisema wakiwa wanazuoni wanaunga mkono maazimio yaliyotolewa na Baraza la Malaigwanani (viongozi wa mila) na viongozi wa siasa ya kutoitambua Kampuni ya Uwekezaji ya Ottler Business Corporation