FLASH


Saturday, February 2, 2013

MTWARA SASA NI SHWARI




Hongera Waziri Mkuu kwa kurejesha utulivu Mtwara


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na waandishi wa habari kwenye makazi yake mkoani  Dodoma jana kuhusu hatua zilizochukuliwa kudhibiti vurugu za gesi mkoa wa Mtwara.Kulia ni waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi.Picha kwa hisani ya gazeti la mwananchi


MOJA ya mambo yaliyoamsha hisia za wakazi wa Mkoa wa Mtwara hadi kushinikiza kwa vurugu wakitaka gesi isitoke mkoani humo, ni taarifa kuwa nishati hiyo ingepelekwa wilayani Bagamoyo, nyumbani kwa Rais Jakaya Kikwete.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema jana nyumbani kwake mjini Dodoma kuwa, mbali na imani hiyo, amebaini pia kuwa mpasuko ndani ya CCM mkoani Mtwara na harakati za kisiasa ni sababu nyingine iliyochochea mgogoro huo.

Pinda alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mgogoro huo ambao ulisababisha vifo vya watu wanne huku wengine wakijeruhiwa vibaya na uharibifu mkubwa wa mali zikiwamo nyumba za wabunge kuchomwa moto na namna alivyofanikiwa kuuzima.

Waziri Mkuu alifanya ziara ya siku mbili mkoani Mtwara, Januari 25 na 26 mwaka huu na kufanikiwa kuzima mgogoro huo baada ya kufanya mazungumzo na makundi mbalimbali ya wadau wa gesi mkoani humo.
“Sasa hili nililitolea ufafanuzi kwa kukanusha kuwa siyo kweli kwamba gesi inakwenda Bagamoyo. Lakini pia baada ya kukaa nao nilibaini kuwa hata viongozi wenyewe wa CCM hawako pamoja,” alisema Pinda na kuongeza:

“Pamoja na hayo nikachukua maelezo kuhusu matatizo yao mengine na nikawaahidi kwamba nitayafikisha katika mamlaka husika ili waweze kuona namna ya kufanya.”

Madai kwamba gesi hiyo inapelekwa Bagamoyo yalikuwa moja ya ujumbe mkuu uliokuwa umeandikwa kwenye baadhi ya mabango wakati wa maandamano ya Desemba 27 mwaka jana yaliyofanyika Mtwara Mjini, yakiratibiwa na baadhi ya vyama vya siasa vya upinzani.

Pinda alisema viongozi wa kisiasa mkoani Mtwara wakiwamo wabunge, wameonekana kuwa na mpasuko unaosababisha uchochezi kwa makundi ya watu.

Alipotakiwa kuzungumzia madai hayo ya Waziri Mkuu, Katibu wa CCM Mkoa wa Mtwara, Alhaji Masoud Mbengula alikiri chama hicho kumeguka na akataja sababu kuwa ni makundi yaliyotokana na uchaguzi wa ndani uliofanyika mwaka jana.

“Tusiwe wanafiki, ni kweli kuna makundi ndani ya chama… wabunge hawako pamoja na ndiyo hali iliyotufikisha hapa… suala hili lipo wazi kabisa,” alisema Alhaji Mbengula.

Kamati ya Spika hatihati
Akizungumzia Kamati ya Bunge iliyotarajiwa kuundwa na Spika kwenda Mtwara kwa ajili ya kuwasikiliza wananchi wa huko, Pinda alisema hawezi kuingilia mhimili huo wa Dola isipokuwa atatoa taarifa bungeni na kama Spika ataona wabunge wameelewa, basi ataamua lolote.

“Nitakuwa na nafasi ya kuzungumzia jambo hili ndani ya Bunge na Spika akiona wabunge wamenielewa bila shaka atasitisha lakini akiona bado inafaa ataamua yeye,” alisema.

Kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari jana, kiongozi huyo alifanya mazungumzo na Mawaziri wanaotoka Mkoa wa Mtwara ambao ni George Mkuchika (Utawala Bora) na Hawa Ghasia (Tamisemi) pamoja na wawekezaji wa kutoka China ambayo alisema yalilenga kuwapa halihalisi ya huko.

Nchimbi afunguka
Akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema vurugu hizo zimefikia mwisho na Serikali haitavumilia tena machafuko ya aina hiyo.

Dk Nchimbi alisema timu ya wataalamu ipo Mtwara kuweka mambo sawa na kusema Serikali itatimiza majukumu yake pasi na shaka yoyote na kusisitiza kuwa haiwezi kukubali Tanzania ikawa vipande.
Alisema Serikali inafanya tathmini kujua hali ilivyo Mtwara na ikibidi itasitisha shughuli zote za kisiasa mkoani humo.

HONGERA SERIKALA YA CCM AMBAPO SASA

Vitambulisho vya Taifa kutolewa wiki ijayo

 

HATIMAYE vitambulisho vya taifa vitaanza kutolewa rasmi siku saba zijazo, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imetangaza.

NIDA imebainisha hayo wakati ujumbe wake ulipomtembelea Rais Jakaya Kikwete, Ikulu jijini Dar es Salaam, kukamilisha taratibu za kitambulisho chake.

Ujumbe huo ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu ulieleza kuwa kuanza kutolewa rasmi kwa vitambulisho hivyo kunatokana na kukamilika kwa utengenezaji huo.
Maimu alimwambia Rais Kikwete kuwa uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho hivyo utafanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam kwa kuanza kuvigawa kwa viongozi wakuu wastaafu.

“Baada ya sherehe hizo za uzinduzi wa utoaji Vitambulisho vya Taifa, maofisa wa NIDA watatoa vitambulisho kwa wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar,” alisema Maimu.

Alimwarifu Rais Kikwete kwamba wanakadiria kutoa vitambulisho kwa Watanzania milioni 21, wenye umri wa zaidi ya miaka 18.

Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete alitaka kujua namna nchi nyingine zinavyoendesha suala la Vitambulisho vya Taifa hasa namna ya kuvitoa bure kwa wananchi.
Maimu alimjibu kwamba kwa Tanzania gharama za Vitambulisho vya Taifa zitabebwa na taasisi zinazotumia habari na takwimu zilizoandaliwa na NIDA.

Kauli hiyo ilionyesha kumfurahisha Rais Kikwete ambaye alisema: “Nawashukuru sana kwa kufikia hatua ya sasa. Tumeanza mbali mno na suala hilo, tangu mwaka 1968. Nafurahi sana kuwa tumefikia mahali pa kuweza kutoa Vitambulisho vya Taifa.”

NIDA ilianza zoezi la kuandikisha wananchi kwa ajili ya kutoa Vitambulisho vya Taifa mwishoni mwa mwaka 2011 baada ya kukamilisha mchakato mzima wa maandalizi.

Awali vitambulisho hivyo vilipangwa Kitambulisho cha kwanza cha Taifa kuwa kimetolewa kwa mtumishi wa umma Aprili mwaka uliopita, lakini ilipofika Novemba, 2012 Maimu licha ya kukiri mpango huo, alisema kwamba ifikapo mwaka 2014 utoaji vitambulisho hivyo utakuwa umekamilika ili viweze kutumika katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na baadaye Uchaguzi Mkuu, mwaka 2015.

Mkurugenzi huyto wa NIDA alitaja sababu za kuchelewa kutolewa kwa watumishi wa umma kutokana na mamlaka yake kukabiliwa na upungufu wa vifaa vinavyotumiwa kuchukua alama na vidole na picha.

Alisema kuwa mamlaka yake ilitakiwa kuingiza mfumo unaotumiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), pamoja na anuani za makazi unaoratibiwa na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).

Zoezi la uandikishaji wananchi kwa ajili ya vitambulizsho hivyo lilianza mwaka uliopita ambapo ulifanyika kwa kanda mbalimbali.

Chanzo mwanachi.co.tz
0
Share