MKUTANO MKUU WA WANACHAMA CCM TAWI MAALUM MZUMBE WAFANA
Tarehe 14.02-2016 mwenyekiti wa ccm tawi maalum chuo kikuu mzumbe ndugu.AHMEDY OMARY Aliitisha mkutano mkuu wa chama ili kujadili ,kujifunza na kukumbushana mambo mbalimbali yanayoendana na miongozo maelekezo ,kanuni,tratibu na katiba ya chama cha mapinduzi
mkutano mkuu huo unafuatia baada ya uongozi mpya kuchaguliwa mapema mwezi uliopita ,pia mkutano huo ulihudhuriwa na mgeni rasmi Mhe.Kingu diwani kata ya mzumbe,pia makada na macomrade mbalimbali wakiongozwa na Malik Malupu,walitoa michango mbalimbali wengine ni Boniphace Maiga ambaye ni mjumbe baraza la vijana mkoa wa Mara na Mlezi UvCCM kata ya Iramba Bunda,Mhe.Yona Habiye,Kimako ambaye pia ni katibu hamasa shirikisho mkoa Morogoro
kikubwa kilichosisitizwa ni kuhakikisha kuwa dhana ya chama inapewa kipaumbele kuliko ubinafsi ,pia kuiishi kwa vitendo kauli mbiu ya SASA KAZI TU,KUIJENGA NCHI NA KUKIJENGA CHAMA
PICHAZA MATUKIO YOTE ZITAPATIKANA HAPA PUNDE.