FLASH


Friday, December 20, 2013

SAFARI YA MWISHO YA KADA MKONGWE WA CCM CLEMENT MABINA

MAGUFULI, WASIRA NA NDIKILO WAONGOZA MAELFU KATIKA SAFARI YA MWISHO YA MWENYEKITI WA ZAMANI WA CCM.Thursday, December 19, 2013

Waziri wa ujenzi John Pombe Magufuli akitoa salamu za rambirambi kwenye ibada ya mazishi ya aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza na Diwani wa kata ya Kisesa hadi mauti yalipomkuta Marehemu Clement Mabina.
Waziri wa ujenzi John Pombe Magufuli akitoa mkono wa pole kwa familia ya Marehemu Mabina.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akito salamu za rambirambi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete kwenye ibada ya mazishi ya Mabina.
Akitoa salamu za rambirambi kwaniaba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarsti Ndikilo amesema kuwa, Rais Kikwete  ametoa pole kwa wananchi wa Kisesa na Mkoa wa Mwanza juu ya tukio hili la msiba wa marehemu Mabina (58) na mtoto Tevery Malemi (12) kutokana na vifo vilivyosababishwa na mgogoro wa ardhi.

Ameongeza kuwa migogoro ya ardhi inapaswa kushughulikiwa kwa uangalifu mkubwa huku hekima na busara zikitumika kushughulikia utatuzi wa migogoro hiyo badala ya kutumia hasira jambo ambalo siku zote husababisha majonzi na madhara makubwa kwa jamii.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Steven Wasira akitoa salamu za rambirambi.
Sehemu ya wanafamilia na viongozi wa Vyama vya siasa na serikali wakishiriki ibada ya mazishi.
Ni sehemu tu ya waombolezaji waliofika katika viwanja vya Red Cross kushiriki ibada hiyo.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Joyce Masunga akitoa salamu za rambirambi.
Mbunge wa Jimbo la Magu naye alitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo.
Katibu wa uhamasishaji wa Chipukizi UVCCM Taifa Paulo Makonda (kushoto) alishindwa kujizuia kuficha hisia zake na kububujikwa na machozi, kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja naye akipiga dua la kumuombe amarehemu Mabina.
Mkuu wa wilaya ya Magu Jackline Liana akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya kamati ya ulinzi na usalama wilayani humo.
Huku akibubujikwa na machozi na kuangua kilio, Mbunge wa Jimbo la Magu Festus Limbu akimpa mkono wa pole mjane wa marehemu Mabina.
Katibu wa uhamasishaji wa Chipukizi UVCCM Taifa Paulo Makonda akiwasilisha salamu za rambirambi.
Askofu Mstaafu wa kanisa la AICT Paulo Nyagwaswa naye alipata fursa ya kutoa neno kwa maelfu ya waombolezaji waliojitokeza leo kwenye ibada hiyo ya mazishi.
Sehemu ya makada wa Chama cha Mapinduzi.
Ulinzi na utaratibu ulizingatiwa na kamati ya mazishi ikiongozwa na Mwnyekiti wa UVCCM Nyamagana Kim.
Ni moja kati ya eneo la mti wa historia ndani ya viwanja hivyo ambapo baadhi ya waombolezaji waliketi wakifuatilia mwenendo wa ibada.
Kusalimiana na kupeana pole kwa viongozi.
Umati ukisubiri kuuaga mwili wa marehemu Mabina.
Uwanjani ilikuwa hivi.
Kutoka juu.
Ndugu wa karibu na marehemu wakiongozwa na baadhi ya watawa kutoka eneo la ibada ya mazishi tayarikuelekea eneo la maziko kitongoji cha Kanyama.
Mbunge Chenge akitoa ushuhuda kwa wanahabari alivyomfahamu marehemu mabina.
Mkurugenzi wa Global Publisher Erick Shigongo akimwelezea marehemu Mabina.
Bodaboda nazo zilitoa huduma ya usafiri.
Sasa ni safari kuelekea makaburini.
Msafara.
Mwili wa marehemu Mabina ukiwasili eneo la maziko kitongoji cha Kanyama.
Ibada ya mwisho kabla ya mazisho eneo la kaburi.
Jeneza la mwili wa marehemu Mabina likishushwa kwenye nyumba yake ya milele.
Viongozi wakiongozwa na Mh. Magufuri wakiweka mchanga kwenye kaburi. 
Mh. Wasira na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Henry Matata wakiweka mchanga kwenye kaburi la marehemu Mabina.
Mjane wa marehemu Clement Mabina,  Bi. Judith Mabina akiweka shada la maua kwenye kaburi la  marehemu mumewe.
Vijana. 
Kumbukumbu.
Kwaheri Clement Mabina, Tunakuombe rehema za Mwnyezi Mungu upumzike kwa amani.