FLASH
Monday, January 28, 2013
MTAZAMO WA KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI CCM TAIFA KUHUSU VURUGU ZA MTWARA
NAPE NNAUYE KAHUSU VURUGU ZA MTWARA
Nimefuatilia
kwa umakini na kuona kuwa Wakazi wa Mtwara na Lindi wanazo hoja za
msingi juu ya suala la gesi, hoja ambazo ni muhimu kusikilizwa na
kupatiwa majibu sahihi..! Lakini nyuma ya hoja hizo muhimu kwa wana
kusini, KUNA WAHUNI, WAHALIFU AMBAO WAMEDANDIA NYUMA YA HOJA NA
KUANZISHA VURUGU, KUCHOMA MALI NA KUHARIBU VITU, Vitendo hivi vya
uvunjaji wa Sheria kimsingi havina uhusiano wa moja kwa moja na hoja za
gesi.
Sisi kama chama tutaendelea kutetea, kutangaza na
kulinda haki za kila mmoja. Dhamira hii inatokana na Katiba yetu lakini
pia inatokana na sera zetu ambazo zinaunda mazingira ya amani na utulivu
katika jamii. Tutaendelea kupiga vita Ubaguzi wa aina zote, Ukabila,
Udini, Rangi, Jinsia na wa Majimbo., ili kujenga na kuimarisha Umoja wa
Kitaifa.
Nasisitiza kuwa “HOJA HALISI” za wanamtwara juu ya
gesi isikilizwe na kupewa majibu sahihi, lakini Serikali iwashughulikie
wahalifu wote ambao wanataka kutumia Suala hili kama kichaka
cha kuendeleza Uharifu na kuvuruga Amani katika nchi.!!. Ni lazima
kusisitiza Utawala unaoheshimu sheria lakini pia kusisitiza juu ya Utii
wa sheria bila shuruti na kuimarisha Uhusiano baina ya vyombo vya dola
na jamii.
Kauli za baadhi ya viongozi na watu wa kawaida
zinaonesha wazi hawana Dondoo sahihi juu ya Suala hili, kauli na matendo
yao vinaashiria mtengano, na kukuza uhasama. Nitoe wito kwa kundi hili,
kuona sababu ya kuifuatilia na kuielewa hoja halisi ya wanamtwara juu
ya gesi, ambayo haisisitizi kujitenga na wala haina asili ya choyo.
Lakini baada ya kuielewa, wasaidie wengine pia kuielewa hoja halisi ya
wana-mtwara inayohoji juu ya maslahi. Ni imani yangu kuwa tutashirikia
pamoja katika Kuimarisha Udugu na Umoja wa kitaifa, na kuwa msitari wa
mbele katika kulinda, kutunza na kusimamia Amani na Utulivu wetu kama
taifa.
Chanzo www.facebook.com/Nape Nnauye
Nimefuatilia
kwa umakini na kuona kuwa Wakazi wa Mtwara na Lindi wanazo hoja za
msingi juu ya suala la gesi, hoja ambazo ni muhimu kusikilizwa na
kupatiwa majibu sahihi..! Lakini nyuma ya hoja hizo muhimu kwa wana
kusini, KUNA WAHUNI, WAHALIFU AMBAO WAMEDANDIA NYUMA YA HOJA NA
KUANZISHA VURUGU, KUCHOMA MALI NA KUHARIBU VITU, Vitendo hivi vya
uvunjaji wa Sheria kimsingi havina uhusiano wa moja kwa moja na hoja za
gesi.
Sisi kama chama tutaendelea kutetea, kutangaza na
kulinda haki za kila mmoja. Dhamira hii inatokana na Katiba yetu lakini
pia inatokana na sera zetu ambazo zinaunda mazingira ya amani na utulivu
katika jamii. Tutaendelea kupiga vita Ubaguzi wa aina zote, Ukabila,
Udini, Rangi, Jinsia na wa Majimbo., ili kujenga na kuimarisha Umoja wa
Kitaifa.
Nasisitiza kuwa “HOJA HALISI” za wanamtwara juu ya
gesi isikilizwe na kupewa majibu sahihi, lakini Serikali iwashughulikie
wahalifu wote ambao wanataka kutumia Suala hili kama kichaka
cha kuendeleza Uharifu na kuvuruga Amani katika nchi.!!. Ni lazima
kusisitiza Utawala unaoheshimu sheria lakini pia kusisitiza juu ya Utii
wa sheria bila shuruti na kuimarisha Uhusiano baina ya vyombo vya dola
na jamii.
Kauli za baadhi ya viongozi na watu wa kawaida zinaonesha wazi hawana Dondoo sahihi juu ya Suala hili, kauli na matendo yao vinaashiria mtengano, na kukuza uhasama. Nitoe wito kwa kundi hili, kuona sababu ya kuifuatilia na kuielewa hoja halisi ya wanamtwara juu ya gesi, ambayo haisisitizi kujitenga na wala haina asili ya choyo. Lakini baada ya kuielewa, wasaidie wengine pia kuielewa hoja halisi ya wana-mtwara inayohoji juu ya maslahi. Ni imani yangu kuwa tutashirikia pamoja katika Kuimarisha Udugu na Umoja wa kitaifa, na kuwa msitari wa mbele katika kulinda, kutunza na kusimamia Amani na Utulivu wetu kama taifa.
Kauli za baadhi ya viongozi na watu wa kawaida zinaonesha wazi hawana Dondoo sahihi juu ya Suala hili, kauli na matendo yao vinaashiria mtengano, na kukuza uhasama. Nitoe wito kwa kundi hili, kuona sababu ya kuifuatilia na kuielewa hoja halisi ya wanamtwara juu ya gesi, ambayo haisisitizi kujitenga na wala haina asili ya choyo. Lakini baada ya kuielewa, wasaidie wengine pia kuielewa hoja halisi ya wana-mtwara inayohoji juu ya maslahi. Ni imani yangu kuwa tutashirikia pamoja katika Kuimarisha Udugu na Umoja wa kitaifa, na kuwa msitari wa mbele katika kulinda, kutunza na kusimamia Amani na Utulivu wetu kama taifa.
Chanzo www.facebook.com/Nape Nnauye
Subscribe to:
Posts (Atom)