FLASH


Sunday, April 14, 2013

UVCCM IRINGA NA MBEYA WAKATAA ZIARA YA VIONGOZI WAO WA KITAIFA

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Hamis Sadifa.
KATIKA mwendelezo wa mnyukano wa hisia za viongozi wa Umoja wa vijana Taifa (UVCCM) kushinda uchaguzi kwa rushwa, baadhi ya viongozi wa umoja huo katika mikoa ya Iringa na Mbeya wameikataa ziara iliyotarajia kufanyika katika mikoa hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wajumbe wa mabaraza ya mikoa na mkutano mkuu wa taifa, walisema kuwa ziara hiyo haina maana yeoyote kutokana na viongozi hao kuwa watuhumiwa wa rushwa.
Baadhi ya wajumbe kutoka mkoa wa Iringa wakiwemo baadhi ya makatibu wa wilaya walisema kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Hamis Sadifa na wenzake ni mmoja kati ya viongozi waliokuwa wanataka kulinda na kutetea ufujaji wa mali za umoja huo mkoani Iringa hasa mradi wa mashamba ambayo mmoja wa viongozi wa umoja huo alikuwa akiutumia kama mali yake binafsi hali ambayo ilipelekea Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa Tumaini Msowoya kusimama kidete na kuhoji hali ambayo akaonekana hafai kwasababu hakutakiwa kuhoji.
Baadhi ya makatibu wa wilaya hiyo walisema kuwa kipindi hiki ni cha kilimo hivyo ziara hiyo haina maslahi kwa vijana wa chama hicho kinachohamasisha vijana kufanyakazi badala ya maandamano na kuzurula kwenye misafara.

Katika mkoa wa Mbeya baadhi ya wajumbe wa baraza la vijana walisema kuwa ziara hiyo hawaitaki kwasababu mbalimbali ikiwemo sababu waliyodai kuwa ni kubwa waliyoitaja kuwa ni ziara hiyo kufedhehesha chama kwa kuwachangisha wadau fedha kwa ajili ya malazi, safari na hata chakula.
walisema kuwa wanatambua kuwa viongozi hao wa kitaifa wanapofanya ziara huwa wanakuwa na mafungu yao lakini wameshangazwa kupata barua na maelekezo kutoka ofisi za mkoa kuwa jukumu la kuwalaza, kuwalisha na kuwasafirisha vigogo hao inabidi zigharamie wilaya kinyume na taratibu huku viongozi wa mkoa wakizidi kuomba michango mpaka huko wilayani ambapo katika wilaya ya Ileje kuna barua iliyokuwa ikielekea kwa Mkuu wa wilaya hiyo ilichanwa.
Baadhi ya wajumbe kutoka wilaya ya Mbeya vijijini walisema kuwa hawapo tayari kuwapokea viongozi hao wa kitaifa kutokana na sababu hiyo na pia mgeni aliyepangiwa kutembelea wilaya hiyo alikuwa ni Makamu Mwenyekiti Taifa Mboni Mwita ambaye tangu uchaguzi mkuu ulipofanyika mjini Dodoma, mkoa wa Mbeya uliongoza kumkataa hata kufikia hatua ya kutaka kupigana na wapambe wake wa baadhi ya mikoa kwa madai kuwa uchaguzi huo ulitawaliwa na rushwa katika nafasi yake hali ilyonusuriwa na usalama wa taifa na msimamizi wa uchaguzi huo William Lukuvi.
Ziara hiyo kwa mkoa wa Mbeya imeelezwa kuwa ingetakiwa kufanyika tangu tarehe 3-4-2013 lakini ikaahirishwa na kupangwa tarehe 13-4-2013 lakini pia imeahirishwa kutokana na kile kilichodokezwa kuwa ni kutokana na baadhi ya vigogo wa umoja huo taifa kuhojiwa na kamati ya maadili.
Hata hivyo ziara hiyo endapo kama itafanyika mkoni Mbeya inaelezwa kuwa itatawaliwa na malumbano kutokana na jinsi ilivyopangwa na kuwakwepesha baadhi ya viongozi wakuu na kuwapeleka katika wilaya za pembezoni ambako vijana wengi hawaweze kuwahoji vema viongozi hao.
Kwa mfano mwenyekiti wa Taifa alipangiwa wilayani Kyela na Mbarali na kumkwepesha Mbeya Mjini ambako inaonekana kuwa Mwenyekiti huyo hana mahusiano mema na Mwenyekiti wa wilaya hiyo aliyetajwa kwa jina la Matukuta huku katibu Mkuu Martin Shigela naye akikimbiziwa Ileje, Momba na Mbozi.

Mbali na viongozi hao kukimbiziwa katika wilaya za nje ya mji, pia hawapo katika ziara ya kuzungumza na wasomi wa vyuo na vyuo vikuu.

Mpaka sasa michngo ya kugharamia ziara hiyo ''mfu'' inaendelea kuchangishwa huku wahusika wakiwa ni makatibu na wenyeviti wa jumuiya hiyo.

Wakati huo huo, taarifa zilizokifikia kikosi kazi cha mtandao wa www.kalulunga.com zimeeleza kuwa katibu wa wilaya ya Mbarali aliyetajwa kwa jina la Mwajuma amejiuzulu na kuacha kazi ya umoja huo kwa madai kuwa anataka kushughulika zaidi na familia yake.