FLASH


Monday, November 18, 2013

KAMERA YETU KUTOKA ZIARA YA CCM HUKO SONGEA

KINANA AKUTANA NA WANA VYUO SONGEA MJINI


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu vya SAUT, St.Joseph na Chuo cha Ualimu Matogoro kwenye ukumbi wa Songea Club.
 Wanafunzi wapatao 650 wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye ukumbi wa Songea Club.
 Mkuu wa Wilaya ya Songea mjini Ndugu Joseph Joseph Mkirikiti(wa kushoto) akiwa pamoja na wadau wa elimu wa Wilaya ya Songea wakimsikiliza Karibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akiwasalimu wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyopo Songea .
 Katibu wa Mkoa wa Vyuo vya Elimu ya Juu Ndugu Christopher Ngubiagai akizungumza na wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini Songea wakati wa kikao cha wanafunzi na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Klabu ya Songea
Baadhi ya wanafunzi wakisikiliza kwa makini masuala mbalimbali yaliyokuwa yanajadiliwa kwenye kikao kilichowahisusha wanafunzi wa vyuo vikuu na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye ukumbi wa klabu ya Songea.