FLASH


Wednesday, April 17, 2013

KILOSA NA GAIRO KWA UFUPI

CCM YAWASHA MOTO LEO GAIRO,


KINANA
GAIRO, MOROGORO, Tanzania
Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo kinatarajiwa 'kuuteka' mji wa Gairo kitakapofanya mkutano mkubwa wa hadhara kuanzia saa kumi jioni katika mji huo.
Kulingana na shamrashamra na simulizi zilizvyotanda miongoni mwa wananchi katika maeneo mbalimbali hapa Gairo, mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na maelfu ya watu, kwa ajili ya kumshudia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ambaye anakuwa Gairo kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake kushika wadhafa huo.
Mbali na Kinana ambaye aliwasili jana jioni, akitokea Kilosa, viongozi wengine wanaotarajiwa kuwasha moto kwenye mkutano huo,ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Dk. Mohammed Seif Khatib.
Kabla ya mkutano huo Kinana na ujumbe wake wamepangiwa kufanya shughuli mbalimbali za ujenzi wa Chama na ukaguzi wa ilani ya CCM, ikiwa ni pamoja na Kinana kufanya kikao cha ndani na  mabalozi na viongozi wa Chama ngazi wa kata zioizopo karibu na makao makuu ya wiyala.
Kaim Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro, Sixtus Mapunda amesema asubuhi hii kiwamba, baada ya mkutano wa ndani, Kinana atafanya shughuli ya kukagua uhai wa chama katika mashina na matawi katika maeneo mbalimbali wilayani hapa


CCM YAFUNIKA KILOSA, MAMIA WAJITOKEZA KUMSIKILIA KINANA

Katibu Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana (kulia) akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara leo jioni mjini Kilosa, mkoani Morogoro.
  Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisaini cha kitabu cha wageni kwenye Shina  la wajasiriamali wakereketwa wa CCM la Dinima, Kilosa katika ya kuwasili mjini Kilosa mkoani Morogoro kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara leo Aprili 17, 2-13.
Vijana wakisahngilia msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, wakati msafara huo ukitoka Ifakara kwenda Kilosa  leo
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akizungumza na wanachama wa CCM shila namba 15, tawi la CCM Mbuni B, Kilosa. Kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi. Alyevaa miwani (kulia) ni Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Dk. mhammed Seif Khatib.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nap Nnauye (kushoto) akimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (kulia) wakati amekaa na wajumbe wa shina  namba  15, tawi la CCM Mbuni B.
Viongozi kuanzia ngazi za mashina wa CCM katika wilaya ya Kilosa, wakizungumza na Kinana kwenye ukumbi wa Comfort, wilayani humo 
Katibu wa NEC, Oganaizesheni Mohamed Sif Khatib akitazama mahidi yalivyostawi kwenye shamba la mkulima maarufu wa wilayani Kilosa

NAPE AWASHUKIA WANASIASA KANJANJA

Katibu Mkuu wa CCM Taifa ndugu Abdulrahaman Kinana akisalimiana na wanachama wa shina la Ulaya Mbuyuni mara tu baada ya kulifungua rasmi ,Kilosa.
Shina hilo ni moja kati ya mashine manne aliyofungua wilayani Kilosa.

Wanachama wa CCM wakiwa kwenye mkutano wa ndani na  Katibu Mkuu wa CCM Taifa,Ndugu Abdulrahaman Kinana.

Wazee waasisi na wanachama hai wa Chama Cha Mapinduzi wakimsikiliza Katibu Mkuu,kwenye mkutano wa ndani hapo Kilosa.

Katibu wa NEC,Oganizesheni, Dr. Mohamed Seif  Khatibu akisalimia wananchi wa Kilosa.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akihutubia wananchi wa Kilosa na kuwapa pongezi kushiriki kwenye  mchakato wa Katiba  Mpya, na pia aliwagusia wananchi kuwa makini na makanjanja wa kisiasa.

Katibu Mkuu wa CCM akihutubia wananchi wa Kilosa na kuwataka kutimiza wajibu,kujiajiri na kuthamini chama cha Mapinduzi.

No comments:

Post a Comment